ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 4, 2020

SHILINGI BILIONI 16 KUWANUFANISHA ZAIDI YA WANANCHI LAKI MOJA WA CHALINZE KATIKA MRADI WA MAJI

 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo wa kwanza akiwa katika  moja  eneo la eneo la chanzo cha maji ya  mto wami na kupokea maelekezo kutoka kwa wataalamu wa Dawasa kuhusiana na mradi huo wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kutembelea miradi mbali mbali ya maji.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akimpa maelekezo moja ya waandisi ambao wanatekeleza mradi mkubwa wa bomba la maji ambalo linatokea katika mitambo ya ruvu juu kuelekea katika maeneo mbali mbali ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo  (PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mtendaji mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja kulia akimpatia maelekezo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo wakati alipotembelea moja ya mradi wa maji ambao utawanufainisha wawekezaji wa viwanda mbali mbali kikiwemo cha kuchakata nyama  katika eneo la Zegereni Wilayani Kibaha.(PICHA NA VICTOR ,MASANGU)
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo kulia akifafanua jambo katika kiwanda cha kuchakata nyama kilichopo katika kata ya Kongowe wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kutembelea miradi mbali mbali ya maji .(PICHA NA VICTOR MASANGYU)
 Mtendaji mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusiana na utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maji katika Mkoa wa Pwani ukiwemo ule wa kutokea katika mtambo wa ruvu juu kuelekea chalinze ambao utagharimu kiasi cha zaidi ya shilingi bilini 16.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Pichani ni moja ya baadhi ya mafundi wakiwa na  mtambo ambao unatumika kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa maji kutoka mtambo wa ruvu juu kuelekea katika maeneo mbali mbali ya Chalinze  Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
  Mbunge wa Jimbo la Chalinze Rizone Kikwete akitoa ufafanua kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani kuhisiana na mwenendo wa ujenzi wa mradi wa maji ambao unateke lezwa na serikali kwa lengo la kuowaondolea changamoto  ya huduma ya maji wananchi.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
VICTOR MASANGU, PWANI
ZAIDI ya wakazi laki moja wanaoishi katika Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani ambao walikuwa na kilio kikubwa cha miaka mingi ya kukosa huduma ya maji safi na salama hatimaye wanatarajia kuondokana na kero hiyo sugu  ifikapo Juni mwaka huu  mara baada ya kukamilika kwa  mradi mkubwa kutoka  eneo la ruvu juu  hadi maeneo mbali mbali ya Chalinze ambao umegharimu kiasi cha zaidi ya bilioni 16.
Hayo yalibainishwa  na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua na kujionea miradi mbali mbali ya ujenzi wa maji katika Wilaya ya Kibaha pamoja na  mradi wa wami ambao upo katika Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo na kuagiza mamlaka husika kuhakikisha wanakamilisha  mradi huo kwa wakati ikiwemo sambamba na kufikishia huduma hiyo katika makazi ya wananchi pamoja na maendeneo yaliyotengwa kwa ajili ya viwanda.
Aidha Ndikilo amezitaka taasisi zote nchini kuhakikisha zinaachana na vitendo vya kuwa ni moja ya vigwazo katika  kuwacheleweshea vibali mbali mbali wawekezaji wa  wa viwanda wa ndani na nje na badala yake washirikiane nao bega kwa bega    katika kutekeleza azma ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
“Kwanza kabisa nimeamua kufanya ziara hii kwa lengo la kuweza kujonenea miradi mbali mbali ya maji katika maeneo ya Mkoa wetu wa Pwani na kwa upande wangu nimeweza kujionea jinsi ya mwenendo mzima, na kiukweli nishukuru sana mtendaji mkuu wa Dawasa pamoja sa safu yake yote kwa kuweza kufanya kazi ambayo inatia moyo ya kutekeleza kwa vitendo miradi ya usambazaji wa maji katika maeneo ya viwandani pamoja na kwa wananchi wenyewe hii ni hatua kubwa sana katika Mkoa wetu,”alisema Ndikilo.
Pia alibainisha kwamba kukamilika kwa miradi mbali mbali ya maji katika Mkoa wa Pwani kutaweza kuwavutia wawekezaji wa viwanda kuwekeza katika miradi mbali mbali sambamba na kuweza kutoa fursa za ajira kwa vijana hivyo amewaomba wamiliki wa viwanda hivyo kuhakikisha wanawapa kipaumbele zaidi wazawa katika suala zima la upatikanaji wa ajira lengo ikiwani ni kujiongezea kipato na kuondokana na wimbi la umasikini.   
Kwa upande wake mtendaji mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja  baada ya kutembelea baadhi ya miradi  ambayo ipo kwenye mpango wa kupatiwa maji ikiwemo viwanda  amesema kwamba lengo lao kubwa ni kuhakikisha kwamba  wanatekeleza kwa vitendo azma ya kumuunga Mkono Rais wa awamu ya tano katika kuwa na uchumi wa viwanda pamoja na kuwaondolea kero wananchi ambayo wamekuwa wakiipata kwa kipindi kirefu kwa  kuwasambazia huduma ya maji safi na salama.
Mhandisi Luhemeja aliongeza kuwa latika jitihada za kuboresha huduma  ya maji katika maeneo mbali mbali Dawasa iliingia mkataba wa ujenzi wa mradi mkubwa wa bomba kuu la kusafirisha maji lenye uumbaro wa kilometa 59 kutoka katika mitambo ya ruvu juu hadi katika kijiji cha Mboga kilichopo katika halmashauri ya Chalinze na utekelezaji wake unaendelea vizuri.
“Ujazo huu wa mradi mkubwa wa kutoka mlandizi hadi chalinze unatarajiwa pindi utakapomalizika utasafirisha kiasi cha lita za ujazo milioni tisa na laki tatu kwa siku moja ambazo zitaweza kuwahudumia wakazi wapatao laki moja na ishirini sambamba na maunganisho mapya ya wateja zaidi ya elfu 18 ambao wataweza kunufaika na mradi huo.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chailzinze  Chalinze Rizone  Kikwete alisema   kwamba wananchi wake kwa kipindi cha miaka mingi wamekuwa na adha kubwa ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama hivyo kukamilika kwa mradi huo utaweza kuwa ni mkombozi mkubwa   katika maeneo mbali mbali ambayo yalikuwa yanakabiliwa na  changamoto sugu ya kutembea umbari mrefu kwenda kutafuta maji katika maeneo mengine ya mbali.
 “Hapo awali wananchi wangu wa chalinze walikuwa wana kero kubwa sana ya kipindi kirefu kutokana na ukosefu wa huduma ya maji, maana walikuwa wanatembea umbari mrefu kwa ajili ya kwenda kutafuta maji lakini napenda kumshukuru sa Rais wetu Dk. John Pombe Magufuli kwa kuweza kutoa kiasi hiki cha fedha ambacho kitasaidia kuleta neema kwa wananchi hawa kwani kwa sasa wao wenyewe wanajionea jinsi ya utekelezaji wa mradi huu na maswali yamepungua kabisa kila kona, alisema Rizone.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani yupo katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili katika baadhi ya Wilaya kwa lengo la kugagua na kujionea shughuli mbali mbali zinazotekelezwa katika miradi  mbali mbali ya maji ambayo imelengwa kuwafikia wananchi pamoja na maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda na mambo mengine.                       

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.