ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 5, 2020

IDADI YA WATALII YAONGEZEKA NCHINI / MAONESHO YA KIMATAIFA YA UTALII KUFANYIKA MWEZI JUNI MWANZA




Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamis Kigwangalla, amesema wizara hiyo kwa mwaka 2018 pekee imepokea watalii milioni 1.5 walioingia na kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo nchini ikiwemo mbuga za wanyama.

 Kauli hiyo ameitoa wakati wa uzinduzi wa maandalizi wa maonesho ya kimataifa ya Utalii kwenye Kanda ya maziwa makuu yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza kuanzia Juni 19 hadi 21 mwaka huu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof Aldof Mkenda akitoa ufafanuzi juu ya kusudio la kufanyika kwa Maonesho ya Utalii ya Kimataifa yanayotarajiwa kufanyika Mwezi Juni 2020 jijini Mwanza.
Mbunge wa Geita mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu ametoa rai kwa wadau kuchangamkia fursa za maonesho hayo ya Kimataifa sanjari na kuonesha bidhaa na huduma zilizokusudiwa kuutangaza utalii na si vinginevyo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Emmanuel Mpawe Tutuba  

Wadau wa Sekta ya Utalii toka mikoa mbalimbali wakisikiliza kwa makini yanayojiri kwenye   uzinduzi wa maandalizi wa maonesho ya kimataifa ya Utalii. Kanda ya Maziwa Makuu yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza kuanzia Juni 19 hadi 21 mwaka huu.
Wadau wa Sekta ya Utalii toka mikoa mbalimbali wakisikiliza kwa makini yanayojiri kwenye   uzinduzi wa maandalizi wa maonesho ya kimataifa ya Utalii. Kanda ya Maziwa Makuu yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza kuanzia Juni 19 hadi 21 mwaka huu.
Wizara ya Maliasili na Utalii imezindua maandalizi ya maonesho ya utalii ya kimataifa na makubwa yatakayofanyika Mwanza mwezi june 2020, Maonesho yanaandaliwa na mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na mkoa wa Tabora na Kigoma kwa lengo la kutangaza vivutio vilivyopo kwenye mikoa hiyo.
Hureeeee.........
Picha ya pamoja.
Picha ya pamoja.
Mwenyeji wa maonesho ya Utalii Kimataifa 2020, Mkuu wa mkoa wa Mwanza John V.K Mongella  akiteta jambo na kamati ya maandalizi kuelekea maonesho ya kimataifa ya Utalii Kanda ya Maziwa Makuu yanayotarajiwa kufanyika mkoani kwake kuanzia Juni 19 hadi 21 mwaka huu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.