ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 3, 2020

ASKARI ZIMAMOTO KIWANJA CHA NDEGE DODOMA KUJENGEWA UWEZO KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA

 Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (ACF) Gilbert Mvungi, akizungumza na Maafisa na Akari wa Jeshi hilo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo Maafisa na Akari wa Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma. Mafunzo hayo yanafanyika katika Ofisi za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma na kuratibiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
 Meneja wa Uwanja wa Ndege Jijini Dodoma Bertha Bankwa (wapili kulia), akimshukuru Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (ACF) Gilbert Mvungi (watatu kulia), Kamishna Msaidizi wa Jeshi hilo ambaye ni Mkuu wa Zimamoto na Uokoaji Viwanja vya Ndege nchini (ACF) Bakari Mrisho (watatu kushoto), Kamishna Msaidizi Mstaafu wa Jeshi hilo (ACF) Christom Manyologa (kulia) kwa kuona haja ya kuandaa mafunzo hayo kwani yataongeza ufanisi katika utendaji kazi kwa Maafisa na Askari hao. Mafunzo hayo yanafanyika katika Ofisi za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma na kuratibiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
 Sehemu ya Maafisa na Akari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wa Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo. Mafunzo hayo yanafanyika katika Ofisi za Jeshi la Zimamoto na Ukuratibiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. 
 Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (ACF) Gilbert Mvungi (watatu kulia waliokaa), Kamishna Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji ambaye ni Mkuu wa Zimamoto Viwanja vya Ndege nchini (ACF) Bakari Mrisho (watatu kushoto waliokaa), Meneja Uwanja wa Ndege Jijini Dodoma Bertha Bankwa (wapili kulia waliokaa), Kamishna Msaidizi Mstaafu wa Jeshi hilo (ACF) Christom Manyologa (kushoto), Mratibu wa mafunzo Uwanja wa Ndege Dodoma Swalha Soka (wapili kushoto waliokaa), Mkuu wa Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Uwanja wa Ndege Dodoma Liberatus Monella (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa na Askari wa Jeshi hilo, baada ya Kamanda wa Mkoa wa Dodoma wa Jeshi hilo, kufungua mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo Maafisa na Akari wa Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma.

Mafunzo hayo yanafanyika katika Ofisi za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma na kuratibiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Aidha imeelezwa kuwa mafunzo hayo yataendelea kwa siku tano mfululizo, na zaidi ya Maafisa na Askari 30 watanufaika na mafunzo hayo pia yataendelea kwa Mikoa mingine kote nchini.

Taarifa ya Jeshi hilo imeeleza kuwa dhumuni la mafunzo hayo kuhakikisha Maafisa na Askari wote wanaohuduma Viwanja vya Ndege kote nchini wanapatiwa mafunzo ya aina hiyo kwa awamu hasa katika kipindi hiki tunapoelekea Tanzania ya Uchumi wa kati unaotegemea Viwanda.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.