ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 17, 2020

MONGELLA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA NIDA MWANZA AKUTANA NA OMBI KWENDA KWA MHE RAIS.


Wakati Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa NIDA ikiendelea na zoezi la usajiri na utambuzi wa raia, nao kupata namba zinazotumika kusajili laini zao za simu kwa alama ya vidole ili kuepuka kuzimiwa mawasiliano, nazo siku za ukomo wa zoezi hilo zikiwa zinatosha hata kuhesabika kwa vidole vya kiganja kimoja, kasi ya uzalishaji wa namba za utambulisho wa Taifa na vitambulisho sanjari na ugawaji wake kwa wananchi umeendelea kuathiri shughuli za ujasiliamali na uzalishaji kwa baadhi yao.

Alhamisi ya tarehe 16 Januari 2020 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella anafanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Mamlaka hizo mkoani hapa ambapo anakutana na misururu ya wananchi wakiwa wamesongamana kwenye mistari kulivaa lango kuu la ofisi hizo kwaajili ya kupatiwa huduma.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.