ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 6, 2020

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA VITUO VYA KISAYANSI PEMBA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Viongozi na Wananchi wa Pujini katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Pujini Wilaya ya Chakechake Kisiwani Pembalepo Januari 06,2020 baada ya kuweka Jiwe la Msingi Kituo cha Ubunifu wa Kisayansi kwa niaba ya Vituo 22 vya Unguja na Pemba  ikiwa ni moja ya Shamrashamra za kuelekea kwenye Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanayotegemewa kuadhimishwa tarehe 12 January 2020 katika Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar.

 Viongozi na Wananchi wa Pujini kisiwani Pemba wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassa wakati alipokuwa akihutubia Wananchi wa Pujini Wilaya ya Chakechake Kisiwani Pemba baada ya kuweka Jiwe la Msingi Kituo cha Ubunifu wa Kisayansi kwa niaba ya Vituo 22 vya Unguja na Pemba leo tarehe 06 Januari 2020 ikiwa ni moja ya Shamrashamra za kuelekea kwenye Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanayotegemewa kuadhimishwa tarehe 12 January 2020 katika Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipata maelezo ya Ujenzi cha Kituo cha Ubunifu wa Kisayansi kwa niaba ya Vituo 22 vya Unguja na Pemba katika Kijiji cha Pujini Wilaya Chake chake Mkoa wa kusini Pemba baada ya kuweka Jiwe la msingi  ujenzi wa Vituo hivyo leo tarehe 06 Januari 2020  ikiwa ni moja ya Shamrashamra za kuelekea kwenye Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanayotegemewa kuadhimishwa tarehe 12 January 2020 katika Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar.Kulia ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Mhe. Simai Mohammed Said.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa Kusini Pemba Mhe. Hemedi Suleiman Abdalla alipowasili Uwanja wa Ndege wa Chakechake kisiwani Pemba leo tarehe 06 Januari 2020  kwa ajili ya kuweka  Jiwe la Msingi Kituo cha Ubunifu wa Kisayansi kwa niaba ya Vituo 22 vya Unguja na Pemba katika Kijiji cha Pujini Wilaya Chake chake Mkoa wa kusini Pemba  ikiwa ni moja ya Shamrashamra za kuelekea kwenye Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanayotegemewa kuadhimishwa tarehe 12 January 2020 katika Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar.

(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.