ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 12, 2019

RAIS MAGUFULI ATANGAZA KUACHIWA KWA NDEGE YA TANZANIA ILIYOKAMATWA CANADA


Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imakamatwa nchini Canada imeachiwa na wananchi watatangaziwa siku ya kuwasili ili waipokee jijini Mwanza.
 
Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa amesema hayo wakati anafungua Semina ya Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) Inayofanyika Jijini Mwanza.

“Kwa taarifa tu, Ndege yetu iliyokuwa imeshikiliwa Canada imeachiwa, mtatangaziwa siku ya kuipokea na itapokelewa hapa Mwanza,” amesema.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.