ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 20, 2019

HOSPITALI YA SEKOU TOURE YAMTUNUKU CHETI MWENYEKIT THE DESK & CHAIR

 Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foundation (TD & CF) Alhaji Sibatin Meghjee (kulia) akimkabidhi hati ya kamabidhiano ya vyoo nane kati ya 20, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure Dk. Bahati Msaki (kushoto) jana.
 Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure Dk. Bahati Msaki (kushoto) jana akimkabidhi cheti Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foundation (TD & CF) Alhaji Sibatin Meghjee (kulia).Cheti hicho ametunukiwa na uongozi wa hospitali hiyo kutokana na kutambua mchango wake kwenye jamii na hospitali yenyewe.
 Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure Dk. Bahati Msaki (kulia) akifungua mlango wa moja ya vyoo vilivyokabidhiwa jana na taasisi ya The Desk & Chair Foundation (TD & CF) tawi la Tanzania.Nyuma ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo alhaji Sibtain Meghjee.
 Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure Dk. Bahati Msaki (kushoto) akifungua bomba na kwenye sinki la maji nje ya vyoo vilivyokabidhiwa jana na taasisi ya The Desk & Chair Foundation (TD & CF) tawi la Tanzania.Kulia ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo alhaji Sibtain Meghjee.
.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure Dk. Bahati Msaki akiflash maji kwenye moja ya vyoo walivyojengwa na taasisi ya The Desk & Chair Foundation (TD & CF) tawi la Tanzania.Picha zote na Baltazar Mashaka 

NA BALTAZAR MASHAKA

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure imemtunuku na kumkabidhi cheti Mwenyekiti wa Taasisi ya The Desk & Cair Foundation (TD &CF), Alhaji Sibtain Meghjeekwa a kutambua mchango wake wa kusaidia jamii.

Alhaji Meghjee alikabidhiwa cheti hicho jana na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dk. Bahati Msaki muda mfupi baada ya hafla ya kukabidhi matundu nane ya vyoo kwenye hospitali hiyo yaliyotolewa na The Desk & Chair Foundation na kugharimu  sh. zaidi ya sh. milioni 20.3.


Akimkabidhi cheti hicho Dk Bahati alisema, Alhaji Meghjee kupitia taasisi hiyo amejitoa na kufanya mambo mengi kwenye  jamii na kujenga miundombinu ya jengo la kupumzikia pamoja na vyoo matundu saba kwa ajili wananchi wanaokuja kuona wagonjwa kwenye hospitali hiyo.

Pia amejenga vyoo matundu manne kwenye jengo la kuhifadhia maiti ikiwa ni pamoja na kutoa msaada waa manteki ya kuhifadhia maji, madawa na vifaa tiba pamoja na mgodoro kwa ajili ya wagonjwa.

“Tutakuwa ni wezi wa wafadhila tusipoenzi na kutambua mchango wa Alhaji Meghjee na taasisi yake katika kusaidia jamii ikiwemo hospitali hii na wapokea huduma wake.Hivyo tunamkabidhi cheti hiki ikiwa ni kumbukumbu yake kwa mazuri aliyotufanyia hospitali ya Sekou Toure,”alisema Dk.

Kwa upande wa alhaji Meghjee alishukuru kwa cheti hicho na kuahidi kitakuwa chachu ya kuendelea kusaidia jamii.

“Najisikia faraja kwa kupata zawadi hii ambayo itakuwa chachu ya kuendelea kusaidia jamii katika sekta mbalimbali kwa kushirikiana na serikali kuhakikisha wananchi wanatimiza ndoto zao,”alisema.  

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.