ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 28, 2019

WATUHUMIWA WA SHEHENA YA DHAHABU MWANZA HUKUMU YATOKA DPP ANENA.



Mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Mwanza imewahukumu wafanyabiashara wanne wa madini ya dhahabu kwa pamoja kutumikia kifungo cha miaka 38 jela au kulipa faini ya shilingi millioni 529.8 baada ya kukiri makosa 9 yakiwemo ya uhujumu uchumi, rushwa pamoja na utakatishaji wa fedha yaliyokuwa yanawakabili.

Hukumu hiyo imetolewa na hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa mwanza Rhoda Ngimilanga  baada ya watuhumiwa hao Sajid Abdalah, Kisabo Nkinda, Emmanuel Kija na Hassan Sadick kukiri makosa yaliyokuwa yanawakabili.
Aidha watuhumiwa wengine wa 8 ambao ni askari polisi wamekana mashtaka yanayowakabili na wamerejeshwa rumande hadi April kumi mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Akizungumza nje ya mahakama Mkurugenzi wa mashtaka nchini Biswalo Mganga anafafanua zaidi. (TIZAMAVIDEO)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.