ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 20, 2018

MKUU WA MOA WA MWANZA ATEKELEZA AGIZO LA RAIS MAGUFULI.


Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe.John Mongella ametekeleza agizo la Rais Mhe. Dkt. John Magufuli la kuhakikisha anafuatilia kero za wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga) na kuzitafutia ufumbuzi.

Katika kutekeleza agizo hilo, Mhe. Mongella amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Sengerema Magesa Mafuru kuhakikisha anakutana na wafanyabiashara wadogo (machinga) ambao walinyang’anywa matunda yao (nanasi) zao kwenye oparesheni ya kuwaondoa barabarani ili walipwe fidia.

Hatua hiyo ilijiri jana Agosti 18, 2018 baada ya Mhe. Rais Dkt. Magufuli akiwa njiani Mjini Sengerema akielekea Chato mkoani Geita kwa ajili ya mapumziko, kutoa agizo kwa watendaji wa halmashauri hiyo kutowasumbua machinga na badala yake wawache wafanye biashara zao huku akiagiza watendaji nchini kujikita kutatua kero za wananchi.

Ni baada ya Mhe. Rais Dkt. Magufuli kusimama kwa ajili ya kusalimiana na wananchi ambapo wafanyabiashara ndogo ndogo walimueleza kero zao ikiwemo ukosefu wa maeneo ya kufanyia biashara zao hatua inayosababisha kubugudhiwa na viongozi wa halmashauri.

Kufuatia malalamiko hayo, Mhe. Rais Dkt. Magufuli alimuagiza Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe. John Mongella kufuatilia kero hizo na kuzitatua ambapo muda mfupi baadaye Mhe. Mongella alikutana na viongozi mbalimbali wilayani Sengerema akiwemo Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na machinga kwa ajili ya kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. Magufuli.
Meza za wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) katika soko la Kisima cha Chumvi Mjini Sengerema ambalo limetengwa kwa ajili ya wafanyabishara hao. Hata hivyo baadhi ya wafanyabiashara wanagoma kuhamia katika soko hili kwa kile wanachodai ni kukosa wateja na hivyo kuendelea kufanyia biashara zao katika hifadhi ya barabara Mjini Sengerema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.