ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 26, 2018

MWANAUME ATUHUMIWA KUMUUA MKE NA MTOTO WAKE WILAYANI CHATO


Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye eneo ambalo kumetokea tukio.

Jirani wa Familia ambapo kumetokea mauaji Bi,Mariam Shija akizungumza na waandishi wa habari kwa masikitiko juu ya tukio hilo.
Diwani wa Kata  Minkoto   , Bw Geroge Magezi akiwasisitiza wananchi kushiriana na jeshi la Polisi kwenye suala la ulinzi na usalama.

Dk Masanja Mchanganya anayetokea kituo cha afya cha Bwanga akielezea namna ambavyo wamebaini mwili wa marehemu majeraha yaliyopo baada ya kufanya uchunguzi.


Na,Joel Maduka,Chato.

Mkazi wa kijiji cha Minkoto Wilaya ya Chato Mkoani Geita Bw Hoja Kasumbakabo ( 25) anatuhumiwa kumuua mke wake Spensioza Petro (22) kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali mwilini na kisha kumnyonga mtoto Brison Hoja mwenye umri wa miezi mitatu kisha   kutokomea kusikojulikana.

Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Leo Nkwabi amesema tukio hilo limetokea tarehe 24 mwezi januari kuamkia tarehe 25 kwenye kijiji hicho ambapo ilibainika miili kuonekana chini ya Sakafu ndani ya chumba walichokuwa wanaishi huku mwili wa mwanamke huyo ukiwa na majeraha sehemu ya kooni, mgongoni na tumboni huku utumbo ukiwa nje.

Mzazi wa marehemu Mzee Petro Lusaga ameelezea kusikitisha na tukio hilo na kwamba hakuwahai kuwaona marehemu na mumewe wakiwa na ugomvi kwani kwa kipindi chote walikuwa wakiishi  kwa amani bila ya kuwa na malumbano wala kelele zozote ndani ya familia yao.

Bi,Judy Masanja ambaye ni jirani wa karibu wa familia hiyo alisema na yeye ameshangazwa na kifo hicho kwani hawakuwai kuwa na ugomvi na siku hiyo walikuwa wamekaa nje na walikuwa wakizungumza vizuri tu hivyo hata  yeye kifo kimekuacha na maswali mengi ya kujiuliza.

Kwa upande wake Diwani wa Kata hiyo, Bw Geroge Magezi amewataka wananchi  kuimarisha ulinzi na kuisaidia serikali kumtafuta mtuhumiwa huku akisisitiza wanaume kuacha mauaji ya namna hiyo.

Dr Masanja Mchanganya anayetokea kituo cha afya cha Bwanga amethibitisha tukio hilo ambapo katika uchunguzi walioufanya wamegundua kuwa marehemu alikuwa na majerahaa matatu makubwa 


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.