ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 26, 2018

KATIBU WA CCM KATA YA BUHALAHALA ATUHUMIWA KUTAFUNA KIASI CHA SH MILIONI 20

Ofisi za  kikundi cha wajasiliamali (KIWAGE) zilizopo mtaa wa Shilabela Mjini Geita  zikiwa zimefungwa .

Mwenyekiti wa Mtaa wa Shilabela   Bw,Elias  Mtoni akielezea suala la vikundi ambavyo vimeonekana kuwa na dhana ya utapeli juu ya fedha za wajalisiamali .

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita,Leornad Kiganga Bugomola akizungumza juu ya uwepo wa taarifa za kiongozi ambaye analalamikiwa kutokomea na fedha za wajasiliamali.
Na,Joel Maduka,Geita...


Katibu wa chama cha mapinduzi CCM kata ya Buhalahala mjini Geita Lazaro Kagoma  anatuhumiwa kutafuna kiasi cha zaidi ya milioni 20 ambazo  zilitolewa na halmashauri ya mji wa Geita kwa kikundi cha wajasiliamali Geita (KIWAGE)walipatiwa na halmashauri ya mji wa Geita.


Kagoma ambaye ni Katibu wa Kikundi hicho cha KIWAGE anadaiwa kuwazunguka wanachama wenzake na kutafuna   fedha walizopatiwa  kwa ajili ya manufaa ya kufanya shughuli za ujasiliamali inadaiwa badala yake alizifanyia matumizi yake binafsi kinyume na matarajio ya kikundi.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Shilabela  Bw,Elias Mtoni  alisema  kikundi hicho kimeonekana kuwa na  ujanja  mwingi kutokana na udanganyifu ambao wameweza kuufanya wa kuidanganya halmashauri  ya mji wa Geita na mwisho wa siku kupatiwa fedha  kiasi cha  Milioni 45.

Shida Mpondi ambaye ni mkazi wa Geita,ameitaka serikali kufanya uhakiki kabla ya kutoa mikopo kwenye vikundi kwa maana ya kujildhihirisha na kujua shughuli ambazo vikundi vinafanya kazi za ujasiriamali ili kuepukana na utapeli wa namna kama hiyo iliyojitokeza.


Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Geita Leonard Bugomola amekiri kupokea malalamiko dhidi ya kikundi hicho huku akisema kwamba Katibu wa Kiwage amekuwa akiwatishia wanakikundi wenzake wanapohoji fedha walizokopeshwa.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti amejibu  tuhuma za kuhusihwa na kikundi hicho kuwa ni mmoja wa watu aliyekipigia chepuo ili kurudisha fadhila katika uchaguzi Mkuu mwaka 2015 jambo ambalo amesema sio sahihi kwani fedha hizo wamekuwa wakikopesha kwa vijana na vikundi ambavyo vimekidhi vigezo pasipo kubagua itikadi ya vyama vya siasa.


Hata hivyo mtandao huu  umewatafuta wahusika akiwemo mwenyekiti na Katibu wa kikundi hicho kwa njia ya simu na simu zilikuwa zikiita bila majibu  huku ofisi za kiwage zikiwa zimefungwa kwa takribani miezi mitano sasa. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.