ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 6, 2018

TETESI ZA WACHEZAJI WANAOWINDWA NA VILABU VYA SOKA ULAYA.

Philippe Countinho
Miamba ya soka ya Hispania Barcelona watalazimika kutoa kaisi cha pauni milioni 145, ili kuweza kupata saini ya kiungo Philippe Coutinho kutoka Liverpool.(Daily Mail)
Wakati huo huo Barca wanakaribia kukamilisha usajili wa beki wa kati Yerry Mina kutoka Palmeirasya nchini Brazil.
Riyad Mahrez kutoka Leicester City iwapo Philippe Countinho.
Majogoo wa Anfield Liverpool huenda wakamsajili winga Riyad Mahrez kutoka Leicester City iwapo Philippe Countinho ataenda Barcelon.. (L'Equipe, in French)
Wapinzania wa jiji la Milan, Inter Milan na Ac Milan wote kwa pamoja wanavutiwa na kumsajili kiungo wa Tottenham Mousa Dembele, mwenye miaka 30.(Sky Sports)
Meneja wa Chelsea Antonio Conte anamatumini klabu yake itafanya usajili mwingine baada ya kumsajili Ross Barkley kutoka Everton.(Independent)
Alexis Sanchez.
Manchester City wanataka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez kwa dau la pauni milioni 35 katika dirisha dogo la mwezi huu wa Januari.
Newcastle United inavutiwa na kumsajili winga wa Kibrazil Kennedy kutoka Chelsea pia wakihitaji kumsajili Danny Ings anayekipiga na Liverpool na pia kocha wa klabu hiyo Rafa Benitez akihitaji kumpa ofa golikipa wa Man City Joe Hart anayecheza kwa mkopo West Ham. (Telegraph)
Southampton wametenga dau la kiasi cha pauni milioni 17.5 ili kumsajili mshambuliaji wa Monaco Guido Carrilo raia wa Argentina mwenye miaka 26.(Sun)
Tottenham wako tayari kusikiliza ofa ya pauni milioni 30 kuuza kiungo Moussa Sissoko ambae amekaa klabuni hapo kwa miezi kumi na nane baada ya kusajiliwa akitokea Newcastle kwa dau la pauni milioni 30.(Daily Mirror)
Radja Nainggolan,
Kiungo wa Ubelgiji ambaye anafukuziwa na Manchester United sambamba na Chelsea Radja Nainggolan, ameonyesha nia ya kucheza kwenye ligi kuu ya China kunako klabu ya Guangzhou Evergrande. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ametaja uwezekano wa kumsaini mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang, 28, kutoka Borussia Dortmund. (Independent)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.