ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 5, 2018

KWA MARA YA KWANZA TUNDU LISSU AFUNGUKA HAYA MBELE YA WANAHABARI NCHINI KENYA.


Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kilichotokea kwake kwa maoni yake ilikuwa ni mauaji ya kisiasa moja kwa moja.

Amesema hayo hivi sasa Ijumaa akiwa anatoka hospitali ya Nairobi nchini Kenya.

“Mimi siyo mfanyabiashara awe amemrusha mtu na huwa hapigani baa,” amesema Lissu.

Amesema kuwa risasi 16 zilimpiga mwili wake huku risasi nane zikitolewa Dodoma na risasi saba kutolewa jijini Nairobi huku akibakiwa na moja mwilini mwake.

Ameeleza kuwa sehemu alipopigiwa risasi ni nyumbani kwake alipopangiwa na Bunge kwa kuwa yeye ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni hivyo eneo ambalo anakaa ni sehemu palipo salama lakini alimiminiwa risasi 16 na waliofanya hivyo hawajulikani walipo.

Amesema kwa watu waliohesabu risasi zilizopiga gari yale ziko 38 lakini 16 ndizo zilizompata mwilini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.