ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, December 3, 2017

MHE MWANJELWA AELEKEZA UONGOZI WA MKOA WA RUVUMA KUHAMASISHA WAKULIMA KUJIUNGA NA VYAMA VYA MSINGI VYA USHIRIKA


 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akikagua Maghala ya Mamlaka ya Taifa ya Hifadhi ya Chakula Kanda ya Songea (NFRA) wakati wa ziara ya kikazi Wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma, Wengine Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe Pololet Kamando Mgema (Kushoto) Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Wa (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba (Katikati) na Meneja NFRA Kanda ya Songea Ndg Amos Mtafya, Jana Novemba 2, 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na kina mama waliojipatia kibara kwenye ujenzi wa Kituo cha mafunzo ya kilimo OTC Lilambo kitakachojihusisha na uchakataji wa mahindi kilichopo Mtaa wa Namanditi, Kata ya Lilambo, Wilaya ya Songea wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Ruvuma, Jana Novemba 2, 2017. 
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa (Wa tatu Kushoto) akitembelea na kukagua Maghala ya Mamlaka ya Taifa ya Hifadhi ya Chakula Kanda ya Songea (NFRA) wakati wa ziara ya kikazi Mkoani Ruvuma, Wengine Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe (Kushoto) Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Wa (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba (Wa Pili kulia) na Meneja NFRA Kanda ya Songea, Jana Novemba 2, 2017. 
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alipotembelea Kijiini Likuyu Fusi, Kata ya Lilambo, Wilaya ya Songea Mjane Bi Ester Gama ambaye ni mke wa Marehemu Leonidas Gama akimvisha kitenge ikiwa ni ishara ya upendo na faraja. Gama alifariki Dunia Novemba 23, 2017 katika Hospitali ya Mtakifu Joseph ya Peramiho.
Jana Novemba 2, 2017.
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua mahindi ili kubaini alipotembelea Maghala ya Mamlaka ya Taifa ya Hifadhi ya Chakula Kanda ya Songea (NFRA) wakati wa ziara ya kikazi Wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma, Jana Novemba 2, 2017.
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akikagua Maghala ya Mamlaka ya Taifa ya Hifadhi ya Chakula Kanda ya Songea (NFRA) wakati wa ziara ya kikazi Wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma, Jana Novemba 2, 2017.

Na Mathias Canal, Ruvuma

Uongozi Wa Mkoa Wa Ruvuma leo Disemba 1, 2017 umeelekezwa kuwahamasisha wakulima kujiunga na vyama vya msingi vya ushirika kwani kupitia vikundi ndio njia muhimu na mkombozi kwa manufaa ya mkulima mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Amebainisha hayo Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa wakati akizungumza na baadhi ya wakulima sambamba na viongozi Wa wakulima katika Mkutano Wa hadhara ulifanyika katika eneo la Ofisi za Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula Kanda ya Songea.

Pamoja na kuwasisitiza wakulima hao kujiunga katika vikundi vya vyama vya msingi vya ushirika, Mhe Naibu Waziri ameelekeza uongozi Wa Mkoa Wa Ruvuma kutilia msisitizo umuhimu Wa Vyama hivyo kwani ni maelekezo ya ilani ya Ushindi ya Chama Cha Mapinduzi katika kipindi cha miaka mitano 2015-2020 inayotekelezwa na serikali ya awamu ya Tano ikiongozwa na Mhe Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Alisema kuwa vikundi hivyo vikianzishwa na kuwa na Uongozi vitarahisisha kuuza mazao mazuri kwani kutakuwa na nguvu ya pamoja inayowakutanisha kwa kuongozwa na sheria na taratibu walizojiwekea kama kikundi pasina kuwa kinyume na taratibu za serikali.

"Upo umuhimu mkubwa Wa kujiunga na AMCOS kwani ni jambo lisilokuwa la hiari ambapo itarahisisha kupata mikopo huku kwa serikali ikiwa ni njia rahisi kuwahudumia, Aidha Elimu inapaswa kutolewa juu ya umuhimu Wa Vyama vya msingi vya ushirika" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Aliongeza kuwa Mamlaka ya Taifa ya Hifadhi ya Chakula nchini inapaswa pia kutoa Elimu kwa umma juu ya majukumu yake kwamba ni kununua mahindi na kuyahifadhi ili kuwa na akiba pindi panapotokea Ukame serikali iweze kuwahudumia.

Awali Naibu Waziri Wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alitembekea na kukagua Ghala La kuhifadhi mahindi Kanda ya Songea ambapo ameshuhudia akiba ya kutosha ya mahindi ambapo mpaka kufikia Leo Disemba 2, 2017 Kanda ya Songea ina mahindi yanayofikia Tani 21,892.924 huku kati yake Tani 10,335.395 ni ununuzi Wa msimu Wa mwaka 2016/2017 na Tani 11,557.529 ni ununuzi Wa mwaka huu 2017/2018.

Aidha, Mhe Mwanjelwa amezuru Kijiini Likuyu Fusi, Kata ya Lilambo, Wilaya ya Songea na kutoa pole kwa Ndugu na Jamaa akiwemo Bi Ester Gama ambaye ni mke Wa aliyekuwa Mbunge na Diwani wa Songea Mjini Mkoani Ruvuma, Marehemu Leonidas Gama aliyefariki Dunia Novemba 23, 2017 Majira ya saa 4:25 Usiku katika Hospitali ya Mtakifu Joseph ya Peramiho iliyopo Songea baada ya kukimbizwa huko kwa matibabu baada ya kuugua ghafla.


MWISHO

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.