ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 10, 2017

IIED NA HAKI MADINI YAWAJENGEA UWEZO WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI MKOANI GEITA.

Baadhi ya wadau wa sekta ya madini Nchini na wachimbaji wadogo wakiwa kwenye mjadala ambao umeandaliwa na Taasisi ya kimataifa ya Mazingirana na  maendeleo(IIED )wakishirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali  hakimadini,Kampuni ya ushauri(MTL) na kituo cha kimataifa cha utafiti wa mistu(CIFOR) na kufanyika kwenye ukumbi wa hotel ya alphendo Mkoani Geita.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ,Mwl Herman Kapufi akimkaribisha mgeni Rasmi kwaajili ya kuzungumza na wadau wa sekta ya madini wakati wa Mkutano wa majadiliano juu ya swala la uchimbaji  madini kwa wachimbaji wadogo.

Kamishina msaidizi wa madini anayeshughulikia wachimbaji wadogo ambaye pia ni mgeni rasimi , Mhandisi David Mulabwa akifungua majadiliano hayo mapema hii leo kwenye ukumbi wa mikutano wa alphendo hotel.

Bw,Fitsum Weldegiorgis ambaye anatoka Taasisi ya kimataifa ya Mazingirana na  maendeleo(IIED ) akielezea namna ambavyo taasisi hiyo imekuwa ikifanya shughuli pamoja na sekta ya madini Nchini.

Rebecca Burton ambaye anatoka taasisi ya Tiffany akizungumza namba ambavyo taasisi yao inafanya kazi wakati wa Mkutano wa majadiliano.

Mtafiti  wa kampuni ya ushauri  Dkt,Willson Mtagwaba,akibainisha changamoto ambazo wamekutana nazo wakati wakifanya tafiti kwa wachimbaji wadogo.

Baadhi ya wadau wa sekta ya madini wakiwa kwenye makundi kwaajili ya kujadili mambo kadha wa kadha.
NA JOEL MADUKA,GEITA



Taasisi ya kimataifa ya Mazingirana na  maendeleo(IIED )wakishirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali  hakimadini,Kampuni ya ushauri(MTL) na kituo cha kimataifa cha utafiti wa mistu(CIFOR) imewakutanisha wachimbaji wadogo wa madini lengo likiwa ni kutazama  na kuona sekta ya madini inavyowahusisha wachimbaji wadogo kwenye shughuli za uchimbaji Mkoani Geita.


Kamishina msaidizi wa madini anayeshughulikia wachimbaji wadogo ambaye pia ni mgeni rasimi , Mhandisi David Mulabwa akifungua majadiliano hayo mapema hii leo kwenye ukumbi wa mikutano wa alphendo hotel,alisema  kuwa tatizo ambalo linawakabili wachimbaji wengi ni kutokuwa na mitaji ya kutosha kwaajili ya kufanya shughuli za uchimbaji kwenye maeneo ambayo yanakuwa na wingi wa madini(MASHAPU).


“Sasa ili kupata wingi wa madini ambayo yapo kwenye Mashapu kunaitajika nguvu kubwa ya mitaji sasa wachimbaji wetu wengi awana mitaji ya kutosha na ndio maana unakuta watu wanachimba tu bila ya kuwa na taarifa za mashapu sasa unapokuwa una taarifa za mashapu ujui unatumia shilingi ngapi na utapata shilingi ngapi  kwa hiyo inakuwa shughuli ya kubahatisha sasa ili uchimbaji uwe wa tija tunawaelimisha ni vizuri wakawa wanatafuta namna ya kupata taarifa za mashapu kwenye maeneo yao”Alisema Mulabwa.


Kwa upande wake Mtafiti  wa kampuni ya ushauri  Dkt,Willson Mtagwaba alibainisha kuwa wakati wa shughuli za kuwazungukia wachimbaji wadogo wamebaini tatizo kubwa wengi wao wamekuwa sio rasmi hali ambayo imeendelea kuleta migogoro baina ya wao na wachimbaji wakubwa na jambo jingine ni kutokuwepo kwa mikopo na bei elekezi.


Bi,Mathar Bitwa ambaye ni mchambaji wa madini ameeleza kuwa bado wanawake wanakabiliwa na changamoto katika sekta ya madini kutokana na kutokupewa kipaumbele kwenye shughuli hizo na kuwepo kwa mila na desturi kwa baadhi ya makabila  pamoja na mfumo dume kwenye shughuli hizo za uchimbaji ,huku Bw, Mtalingi Hamza Mohamedi akielezea sababu ambazo zinasababisha kutokupewa mikopo na mabenki ni kutokana na wao kutokujua kile ambacho wanakichimba wakati wa shughuli hizo.


Naye Mkurugenzi wa taasisi ya hakimadini,Bw Amani Muhina alisema kuwa uchimbaji mdogo unatoa fursa sawa kwa  watu kubadilisha maisha yao bila kuwa na ubaguzi wa kipato au Elimu kwasababu uchumi wa nchi unaletwa na watanzania wenyewe.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.