Baadhi ya
vikundi vya wajasiriamali wakiwa katika
picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya
Kisarawe wakati wa sherehe za kukabidhiwa hundi ya kiasi cha shilingi milioni 102
kwa ajili ya mikopo ambayo iatawasaidia katika kuendeshea shughuli zao za biashara pamoja na
ujenzi wa viwanda vidogo vidogo. (PICHA NA VICTOR MASANGU)
Mkuu wa
Wilaya Kisarawe Happiness Seneda
aliyesimama akizungumza na vikundi vya wajasiriamali kutoka kata mbali mbali
katika halfa fupi ya kukabidhiwa hundi ya kiasi cha shilingi milioni 102 kwa
ajili mkopo wa kuwawezesha kiuchimi.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Happiness Seneda akizungumza jambo katika halfa fupi ya vikundi vya wajasiriamali.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashari ya Kisarawe Mussa Gama akizungumza na vikundi vya wajasiriamari hao hawapo pichani kabla ya kukabidhiwa hundi hiyo ya kiasi cha shilingi milioni 102 kwa ajili ya kuwawezesha mikopo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)
NA VICTOR MASANGU, KISARAWE
HALMASHAURI YA wilaya ya Kisarawe
iliyopo Mkoani Pwani
katika kuunga mkono juhudi za Rais wa
awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli kuwa na uchumi wa viwanda imetoa
kiasi
cha shilingi milioni 102 kwa vikundi vya wajasiriamali vipatavyo 49 vya
wakinamama,vijana pamoja na walemavu kwa lengo la kuweza
kuwasaidia kuendesha shughuli zao mbali
mbali za biashara mbali mbali
ikiwemo na kuwawezeha ili waweze
kujikita zaidi katika kujenga viwanda
vidogo vidogo.
Akizungumza katika halfa fupi ya kukabidhi hundi ya fedha hizo iliyohuduriwa na viongozi
mbali mbali wa serikali pamoja na viongozi wa vikundi hivyo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya
ya Kisarawe Mussa Gama alisema kwamba fedha
hizo za mikopo zimetolewa kwa vikundi
hivyo kutokea kata zote 17 ambapo zimetokana na makusanyo ya mapato ya ndani.
Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa kutaweza kuleta mabadiliko
chanya ya kimaendeleo na kuweza kukuza uchumi wa nchi
kutokana na kuweza kuwapa fursa wajarisiamali hao kupania wigo wa
kibiashara pamoja na kuanzissha viwanda vingine vidogo vidogo ambayo vitaweza kuongeza upatikanaji wa ajira
mpya na kupunguza wimbi la umasikini.
“Kwa kweli sisi kama halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe
tumejipanga kuweka mipango madhubuti katika kuviwezesha vikundi vyetu vya
ujasiriamali kwa kutumia fedha zetu ambazo zinatokana na makusanyo ya mapato ya
nadani, hivyo vikundi hiivi ni moja ya mipango yetu katika kuhakikisha ile
asilimia 10 iliyotengwa inawafikia walengwa na kuweza kuleta mabadiliko chanya
ya kimaendeleo,”alisema Mkurugenzi huyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Happiness Seneda
ameviasa vikundi vyote vilivyopata mkopo huo
hususan kwa wakinamama kuachana kabisa na vitendo vya kutumia fedha hizo vibaya kwa shughuli ambazo
hazina manufaa yoyote kwa jamii, kama vile kuwachezesha watoto
wao ngoma wakati wa kufunga shule
pamoja na kununulia madela kitu ambacho amekilaani vikali.
Aidha Seneda alisema kuwa malengo ya serikali ya awamu ya
tano ni kuhakikisha wananchi wake wanawezeshwa kwa namna mbali mbali ikiwemo
kuwapatia mikopo ambayo itaweza kuwapa fursa ya kukuza biashara zao pamoja na
wengine kufanya biashara zao ndondogo amabzo zitaweza kuwapatia kipato na
kujikwamua kiuchumi.
“Jamani mimi kama kiongozi wenu napenda kuwaasa wale wote
mlionufaika na mkopo huu, kuhakikisha mnazitumia vizuri fedha hizi hasa kwa
upande wa wakinamama ambao wamekuwa na tabia pindi wanapotata pesa wanazitumia
katika matumizi mengine ya kununulia madela kwa ajili ya sare pamoja shughuli
nyingine kama vile kuwacheza ngoma watoto wao hii tabia kwa kweli sipendi
kuiona katika Wilaya yangu,”alisema Seneda.
Nao baadhi ya wajasiriamali ambao wamenufaika na mkopo wa
fedha hizo akiwemo Monica Muhoza ambaye ni mlemavu wa miguu,
Faudhia Kasikasi, pamoja na Gudluck
Akyoo wameshukuru uongozi mzima wa
halmashauri ya Kisarawe na kusema kuwa fedha hizo walizopatiwa ni mkombozi mkubwa kwa upande
wao kwani zitaweza kuwasaidia kujikwamua
kiuchumi pamoja na kujikimu kimaisha na kuendesha familia zao.
VIKUNDI hivyo vya wajasiriamali 49 kutoka kata 17 za
Wilayani Kisarawe zimewahusiha wakinamama, vijana, pamoja na makundi vya walemavu
ambapo vimepata mkopo wa fedha hizo kiasi cha shilingi milioni 102 ikiwa ni
makusanyo ya mapato ya fedha za ndani.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.