ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 22, 2017

ZSSF YATILIANA SAINI NA BANKI TPB BANK UTOWAJI WA MIKOPO KWA WANACHAMA WA ZSSF ZANZIBAR.

MKURUGENZI Mkuu wa Tpb Bank Sabasaba Moshingi kushoto na Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Jamii Zanzibar (ZSSF) Makame Mwadini wakitiliana saini makubaliano ya kutowa mikopo ya Kielimu na Kuazia Maisha kwa Wanachama wa (ZSSF)hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa ZSSF kilimani Zanzibar, wakishuhudia Mwanasheria wa ZSSF Mohammed Fakih na Afisa Mawasiliano wa Tpb Bank Chichi Banda
Mkurgenzi Mkuu wa Tpb Bank Sabasaba Moshingi kushoto akibadilishana mikataba wa mikopo kwa Wanachama wa ZSSF kupata mikopo kupitia Banki ya Tpb Bank, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Mwadini Makame,  kuwawezesha kupata Mkopo wa Elimu ya Juu na kuaza maisha kwa Wanachama wa ZSSF, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Kilimani Zanzibar.wakiwa katika picha ya pamoja na Maofisa wa pande hizo mbili.
Maofisa wa Tpb Bank wakifuatilia mkutano huo wa utilianaji saini ya kutowa mikopo kwa Wanachama wa ZSSF Zanzibar kupitia benki hiyo hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi za ZSSF Kilimani Zanzibar.
Maofisa wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF wakifuatila mkutano huo wa utilianaji wa saini.
Afisa Mawasiliano wa Tpb Bank Chichi Banda akitowa nafasi kwa waandishi wa habari kuuliza maswali wakati wa hafla hiyo.
Mkurgenzi Mkuu wa Tpb Bank Sabasaba Moshingi, akizungumza wakati wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini kuelezea madhumuri ya hafla hiyo kuwanufaisha Wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar kupata mikopo kupitia Banki yake Tpb Bank. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Mwadini Makame
akizungumza wakati wa hafla hiyo ya makubaliani ya kupata mikopo kwa Wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF, kupitia Banki ya Tpb Bank.
Maofisa wa Tpb Bank wakifuatilia hafla hiyo ya utilianaji wa saini na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF. 
Mwandishi wa habari akiulisa swali wakati wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini baina ya ZSSF na Tpb Bank, kutowa mikopo kwa Wanachama wa ZSSF kupata Elimu ya Juu na Mkopo wa kuazia maisha. 
Mwandishi wa habari akiuliza swali wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi Mikopo wa Banki ya Tpb Bank Ndg. Henry Bwogi akifafanua na kujibu maswali yalioulizwa na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo ya utilianaji wa saini baina ya pande hizo mbili. 
Afisa Masoko na Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF Bi Raya Hamad Khamis akitowa shukrani kwa washiriki wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini uliofanyika katika Ofisi za Jengo la ZSSF Kilimani Zanzibar. 
Viongozi wa Tpb Bank na ZSSF wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa hafla hiyo. 
Mkurugenzi wa Banki ya Tpb Bank Sabasaba Moshingi akiwa na Maofisa wa ZSSF wakibalishana mawazo baada ya kumaliza hafla ya utilianaji wa saini na ZSSF, katikati Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZSSF Ndg.Mwadini na Afisa wa ZSSF Miradi Ndg. Muumin.
Mkurugenzi wa Banki ya Tpb Bank Sabasaba Moshingi akisalimiana na Afisa wa ZSSF Ndg Filifili. 
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.com
Zanzinews.com.
Email. othmanmaulid@gmail.com
0777424152. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.