Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera
Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Amantius Msole na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Steven Makonda.
Katika taarifa ambayo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imeeleeza kuwa sababu ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wao ni baada ya kubaini kuwa wamefungua akaunti nyingine ya benki kwa kutumia jina linalofanana na akaunti rasmi ya kuchangia maafa iitwayo ‘Kamati Maafa Kagera’ kwa leno la kujipatia fedha.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.