ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 3, 2015

SKYLIGHT BAND KUSINDIKIZA TAMASHA LA FAHARI YA MWAFRIKA NDANI YA KIOTA CHA ESCAPE ONE LEO JUMAMOSI

Mmiliki wa Skylight Band Dk Sebastian Ndege(Jembe ni Jembe) akicheza moja ya nyimbo ya bendi Skylight. Njoo leo Jumamosi kwenye Show ya Fahari ya Mwafrika itakayofanyika kwenye kiwanja cha Escape One ambapo Skylight Band ikisindikizwa na Msanii machachari Barnaba Classic watadondosha moja ya show kali usisubirie kusimuliwa njoo wewe na yule.
Sam Mapenzi pamoja akiimba kwa hisia kali mbele ya mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani) waliofika kwenye kiota cha Escape One Mikocheni.
Ashura Kitenge (kushoto) akiwa na Kasongo Junior wa Skylight band waiimba na kucheza mbele ya mashabiki wao ndani ya kiwanja cha Escape One Mikocheni
Sony Masamba akiendelea kutoa burudani huku akisindikizwa na waimbaji wenzake ndani ya kiota cha Escape One siku ya Jumapili iliyopita.
Burudani ikiendelea
Mwimbaji wa bendi ya Skylight Natasha akiwapa mashabiki vionjo vya nyimbo za taratibu na kutoa burudani ya nguvu kwa wapenzi wa bendi hiyo waliofika siku ya Jumapili ndani ya Kiota Cha Escape One.
Bendi ya waimbaji wakali wa Skylight ikirindimisha baadhi ya nyimbo zao huku wakiendelea kuzirudi nyimbo kali za Bendi hiyo
Sam Mapenzi akitoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake ambao ni Sony Masamba(kushoto) na Kasongo Junior(kulia).
Bendi ya waimbaji wakali wa Skylight ikirindimisha baadhi ya nyimbo zao
Sam Mapenzi pamoja(Kushoto) na Ashura Kitenge wakiimba kwa furaha huku wakikonga nyoyo mashabiki wa Skylight Band waliofika kwenye kiwanja cha Escape One, Mikocheni
Kushoto Rapa mkongwe katika muziki wa Live Joniko Flower pamoja na mwenzake Sony Masamba wakisababisha mashabiki viuno vyao viweze kuzungushwa mithiri ya feni.
Ilikuwa noma sana siku ya Jumapili iliyopita maana ilikuwa sio ya kupitwa basi mchuke na ndugu, jamaa au rafiki yako leo uje kuona vitu vitamu kutoka kwenye Bendi ya Skylight
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akishusha mistari na kucheza huku waimbaji wenzake Sony Masamba (wa pili kutoka kushoto), Ashura Kitenge(wa pili kutoka kulia) pamoja na Sam Mapenzi wakisebeneka
Wanaume wa shoka wakilisakata rhumba wakati wa kuwafurahisha mashabiki wa bendi ya Skylight
Bendi haiwezi kuwepo bila kuwa na hawa jamaa wakali wanaosababisha Bendi ya Skylight kupaa
Ule muda sasa ulifika wa kusugua maana ilikuwa ni noma sana
Wanaume wa shoka wakilisakata rhumba wakati wa kuwafurahisha mashabiki wa bendi ya Skylight
Mashabiki wa Bendi ya Skylight wakiendelea kukata mauno kutokana na muziki mkali wa bendi hiyo jumapili iliyopita.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.