ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 22, 2014

AIRTEL YAJA NA 'SWITCH ON' Intaneti maalum kwa simu unayotumia.

Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Tanzania, Levi Nyakundi akizungumza na wadau mbali mbali (hawapo pichani) waliohudhulia hafla hiyo ya uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel kwa watumiaji wa Internet hapa nchini ijulikanayo kama SWITCH ON. hafla ya uzinduzi ilifanyika jana usiku katika  Hoteli ya Hyatt Agengy The Kilimanjaro,Jijini Dar es Salaam.
Mabalozi wa Huduma mpya ya Airtel ya ‘SWITCH ON’ wasanii maarufu Ney wa Mitego, Vannessa Mdee na Barnabas wakiwa wameshikilia mabango yenye kuonyesha namba ya kujiunga na huduma hiyo ya intaneti wakati wa hafla ya uzinduzi wake uliofanyika jana usiku kwenye kiota cha Maraha cha Club Rouge ndani ya Hoteli ya Hyatt Agengy The Kilimanjaro,Jijini Dar es Salaam.
Msaanii maarufu kwa kumiliki jukwaa na balozi wa huduma ya Airtel SWITCH ON Vanesa Mdee akiwa na wacheza shoo waki wakitoa burudani kali kwa wageni waalikwa  waliohudhulia hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel kwa watumiaji wa Internet hapa nchini ijulikanayo kama SWITCH ON. hafla ya uzinduzi ilifanyika jana usiku katika  Hoteli ya Hyatt Agengy The Kilimanjaro,Jijini Dar es Salaam.
Msaanii maarufu na mwenye uwezo wa kutumia gitaa na kuimba pia ni Balozi wa Airtel SWITCH ON barnabas  akitoa burudani kali kwa wageni waalikwa waliohudhulia hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel kwa watumiaji wa Internet hapa nchini ijulikanayo kama SWITCH ON. hafla ya uzinduzi ilifanyika jana usiku katika  Hoteli ya Hyatt Agengy The Kilimanjaro,Jijini Dar es Salaam.
Airtel yaja na SWITCH ON, Intaneti maalum kwa simu unayotumia

·        Airtel yazindua huduma ya kipekee ya vifurushi vya data maalum kwa simu na mahitaji ya kila mteja.
·        Airtel kuwapa suluhisho bora wateja katika huduma ya Internet
·        Wateja wa Airtel kufurahia inteneti bora kwa gharama nafuu

Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel leo imezindua huduma kabambe ya Intaneti itakayojulikana kama SWITCH ON. Huduma hiyo ni maalum kwa watumiaji wa huduma za Interneti Tanzania ambapo sasa wateja wa Airtel wataweza kufuruhai huduma ya kipekee ya vifurushi vya data/intaneti maalum kwa simu na mahitaji ya kila mteja.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel  Tanzania Bw, Levi Nyakundi alisema “ ulimwengu wa leo matumizi ya huduma za intaneti/data au mtandao hayaepukiki, ukitaka kujua kinachoendelea duniani kwa haraka basi intaneti ndio suluhisho au jawabu linapopatikana, lakini kumekua na changamoto nyingi sana hasa pale tunapohitaji intaneti bora ya kutuwezesha kufanya fasta mawasiliano na tuwapendao au tunapotaka kuunganishwa na taarifa za mambo muhimu yanayoendelea dunia kote, inawezekana kila wakati umekua ukijiuliza ni MB au GB au kifurushi gani kitakuwezesha kufanya mambo yako kuwa poa zaidi, hili ndilo lililotusukuma Airtel kukuletea wewe mteja wetu huduma hii ya kisasa na ndio maana tunakuambia SWITCH ON”

“Ukiwa na Airtel ‘SWITCH ON’ watumiaji wa huduma za Intaneti Tanzania sasa wanakila sababu yakufurahia kujipatia huduma bora zaidi kwa gharama nafuu na kufanya chaguo la kufurushi utakacho MAALUM kwa simu yako. Hii ni huduma inayoenda na wakati, inazingatia utamaduni wetu kwa kuwa ni ya kukutoshelezea hitaji lako, na gharama ni nafuu kuliko zote huku ikikuhakikishia mteja Non-stop intaneti - yaani fulu makamuzi kwa wewe mtumiaji kutokupimiwa. Huduma hii ya pia inamuwezesha mteja kuwa na chaguo la kifurushi iwe kwa SIKU, WIKI auMWEZI”

“Airtel Tanzania tumejipanga zaidi kuhakikisha tunaendelea kuwa wabunifu na kuwapatia huduma bora ya mawasiliano ya internet. Tutaendelea kufanikisha  hili kwakuwa Airtel Yatosha, Airtel Money nusu gharama, au Bure Pack ni vielelezo vya huduma bora na nafuu tunazowapatia wateja wetu kwa sasa na kuwafaidisha wateja kila siku. Hivyo leo hii SWITCH ON nimuendelezo wa kuwahudumia watumiaji wa Internet nchini Tanzania kwa kuwapa wanachokitaka bila kikwazo yaani Fulu makamuzi” aliongeza Nyakundi 
 Kwa upande wake Meneja Masoko wa Airtel Bi Prisca Tembo akielezea jinsi ya kutumia huduma hiyo alisema “Ni rahisi sana mteja wetu kujiunga, unatakiwa tu kupiga *148*22# ikiwa tu una simu yako yenye uwezo wa kutumia intaneti /Data kisha utaweza kujichagulia aina ya kifurushi kinachokufaa kutokana na mahitaji yako kwa kuwa vifurushi ni maalum kwa simu au kifaa utakachotumia yaani iwe unasimu ya Feature phone, au Simu mpapaso (Smart phone au Tablet sisi Airtel tumekuwekea kifurishi cha intaneti maalum kwa kila simu”

‘Vilevile kwa wale wateja wote wa Airtel wanaotumia huduma ya Airtel Yatosha pia bado wananafasi ya kujiunga na vifurushi vya intaneti vya Yatosha na ikiwa wamemaliza Data /intaneti na wanapenda kujiunga na Data pekee basi wanaweza pia KU-SWITCH ON na kuendela na makamuzi” alimalizia kusema Prisca.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.