ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, November 11, 2013

ATHARI ZA BIASHARA YA VYUMA CHAKAVU JIJINI MWANZA.

LEO nikiwa katika mishemishe zangu jijini hapa nayo macho nikiyaelekeza chini kukagua njia niipitayo kuepuka madimbwi ya maji, matope na mashimo ya hapa na pale, macho yangu yanashuhudia hali hii kwenye mashimo ya viunganishi vya maji taka pembezoni mwa barabara ya Nyerere. Hebu safiri nami.
Pamoja na kuweka kufuli wameng'oa mfuniko.
Mzigo mwingine wa hapa umekwenda.
Ngoma nyingine hiyo imesepeshwa...
Hapa panaliwa 'taiming'.
Salama ya hili ni kwamba liko mbele ya Bank.
Hili liko mbele ya sheli lakini sementi iliyolishikilia inaendelea kulika pembezoni ni mkono wa mtu au tabia nchi?
Hivi ndivyo mifuniko ilivyo wekewa ulinzi.
Sasa hapa wamelamba hadi kufuli....Dadeki..!!
Hii hi barabara ya Nrerere vipi hali ya barabara nyingine za kwetu Uswazi?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.