ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 1, 2011

BURIANI SALUM KABUNDA 'NINJA'

Aliyekuwa beki wa zamani wa Dar es salaam Young Africans Salum Kabunda 'Ninja' amezikwa leo kwenye makaburi ya Kirumba jijini mwanza.Hayati Salum Kabunda 'Ninja'.

Salum kabunda aliaga dunia jana ijumaa majira ya usiku saa 2 na robo akiugulia nyumbani kwa mama yake mzazi mtaa wa Nela jijini hapa. Marehemu ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto wa 5 wa familia ya Mzee Hassan kimwaga ameacha mjane na watoto wanne akiwemo Hassan Kabunda ambaye yuko katika kambi ya michezo ya Kanali Kipingu.

Timu alizopitia ni pamoja na Dar es salaam Relwe, Waziri mkuu Dodoma ambako aliungana na akina Godwin Aswile kisha baadaye wakachukuliwa na tajiri mmoja na kuelekea Tukuyu Stars ya Mbeya ambako Yanga iliwanasa na kuwasajili.

Marehemu Salum Kabunda Ninja' aliisaidia timu ya Taifa iliyoitwa 'Kakakuona' kufika faina ya CECAFA Senior ambapo walipoteza mbele ya Uganda kwa kufungwa 1-0 Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza kabla ya kuiwakilisha vyema Tanzania katika mchezo dhidi ya Zambia 'Chipolopolo'

Alitunukiwa jina Ninja kutokana na ufanisi wake kama beki kwa kuweza kuruka style mbalimbali kuondosha hatari langoni mwa timu yake ya Yanga akifananishwa na wacheza filamu maarufu ya miaka ya 90' 'Ninja'

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amen

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. You are going to sреnԁ that money any way to get the items fоr free.
    You can now chаnge the proxy sеttіngѕ via Uрdаte
    sеttings in VIPRE. The daytime activіtieѕ we decided to add were 2 tiсkets on the Gatlinburg Sky Lіft and
    a 1 houг romantiс horseback ride.


    Feel free tο viѕit my hоmepage: http://Www.caminoalislam.Com

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.