ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 5, 2011

TBL YAZINDUA KAMPENI YA JIVUNIE UTANZANIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Tanzania,Robin Goetzche akizungumza leo katika uzinduzi wa Kampeni ya Jivunie Utanzania inayoendeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro Lager ikiwa ni harakati ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.Kampeni hii imezinduliwa leo hii katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa,katikati ya Jiji la Dar na kuhudhuriwa na wageni mbali mbali.

Suleiman Nyambui akiwaeleza jambo waandishi wa habari.

Wakongwe wa Muziki wa dansi nchini pia walikuwa ni sehemu ya wageni waalikwa katika hafla hiyo.

Wachezaji wa zamani wa timu za mpira wa miguu wa timu za Yanga na Simba pia walikuwepo.toka kushoto ni Salvatory Edward,Kenneth Mkapa,Mohamed Mwameja na Edbil Jonath Lunyamila.

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akiwa katika mazungumzo na Mkuregenzi wa Bodi ya TBL, Arnold Kileo pamoja na Mjumbe wa Bodi ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Ali Mwaimu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.