Mabadiliko ya Tabia nchi ndilo sasa tatizo linaloleta changamoto kubwa sana duniani hasa katika ukuaji wa uchumi, ustawi wa jamii na maendeleo endelevu kwa bara la Afrika.
Asilimia 75 ya watoto wanaokufa kwa maralia inatokana na uchafuzi wa maralia;
Kwa upande wa Tanzania tayari athari zimeanza kujitokeza, kina cha maji Ziwa Victoria kimepungua kwa mita 2.57, Ziwa Rukwa limepungua kwa kilomita 7 kwa kipindi cha takribani miaka 50 iliyopita. Kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari baadhi ya visima vya maji safi katika mwambao wa Pwani ya Bagamoyo na Pangani sasa vimeingiliwa na maji ya chumvi na vingine havitumiki kabisa hivyo kuathili upatikanaji wa maji safi na salama.
Nchi yetu pia inashuhudia kuenea zaidi kwa ugonjwa wa maralia katika maeneo ambayo haukuwa kawaida kama maeneo ya mkoa wa Kagera, Mbeya, Lushoto na Amani mkoani Tanga.
Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, inaendelea kuelimisha umma na wataalamu katika sekta na taasisis za umma pamoja na sekta binafsi kuhusiana na tatizo la mabadiliko ya Tabianchi na kujiandaa vyema kukabiliana na tatizo kwa ujumla.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.