.jpg)
Mwandishi wa habari wa mkoa wa Kigoma, Editha Karlo, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Kigoma, Jacob Ruvilo, aliyesema kuwa marehemu alifariki Jumatano mchana Aprili 28,2026 akiwa nyumbani kwao wilayani Kasulu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kabla ya umauti wake marehemu alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Kifo cha Editha Karlo ni pigo kwa familia, ndugu, marafiki na tasnia ya habari mkoani Kigoma na nchini kwa ujumla.
Tupe maoni yako
.jpg)
0 comments:
Post a Comment