ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, April 26, 2026

'LEO WANAUME WA MWANZA MMEFIKIWA' KARIBU KIKAONI

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Jumapili hii, yaani LEO - tarehe 26 Aprili 2026, jiji la Mwanza linakuwa kitovu cha mjadala muhimu unaomhusu mwanaume wa kizazi cha sasa. Ndani ya Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT – Capri Point), tukio maalum la Mwanza Wanaume Summit 2026 linafanyika, likiwaleta pamoja wanaume kutoka pande mbalimbali za Kanda ya Ziwa na kwingineko. Kuanzia saa 8 mchana hadi saa 12 jioni, washiriki watapata fursa ya kipekee ya kujifunza, kuhamasishana na kujenga mtazamo mpya unaoendana na changamoto na fursa za maisha ya leo kuanzia majukumu ya kifamilia hadi mchango wao katika jamii na taifa. Katika mazungumzo haya yenye uzito, Maxwell Stanslaus Shing’oma, Rais wa Taasisi ya Wanaume Tanzania (Men At Work Global), anafungua pazia kwa kueleza kwa kina dhamira ya kongamano hili na kwa nini ni muhimu kwa maendeleo ya mwanaume wa kizazi hiki.......

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment