ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 17, 2026

KOCHA BILO AFARIKI AKIWA UWANJANI JIJINI MWANZA

aa

  Athuman Bilali maarufu kama Billo.

Picha: Mtandao
Athuman Bilali maarufu kama Billo.

Aliyewahi kuwa kocha wa timu mbalimbali za soka nchini, ikiwamo Stand United ‘Chama la Wana’ na Pamba (sasa Pamba Jiji), Athuman Bilali maarufu kama Billo, amefariki dunia huku chanzo cha kifo chake kikiwa bado hakijafahamika.

Marehemu Billo hadi mauti yanamkuta alikuwa mmiliki wa kituo cha michezo pamoja na timu ya wanawake ya Bilo Queens inayoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania.

Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA), Leonard Malongo, amethibitisha kifo hicho, akieleza kuwa ni pigo kubwa kwa wadau wa soka mkoani Mwanza na nchini kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Malongo, taarifa za awali zinaeleza kuwa kocha huyo aliendelea na majukumu yake ya kawaida ya mazoezi na timu ya Bilo Queens katika Uwanja wa Shule ya Msingi Nyasaka jijini Mwanza hadi jioni ya Aprili 15, 2026. Hata hivyo, baada ya wachezaji kuondoka, aliachwa akiwa amekaa uwanjani na baadaye alikutwa amefariki eneo hilo asubuhi iliyofuata.

“Jana alikuwa uwanjani akifanya mazoezi na timu yake, lakini hadi wachezaji wanaondoka walimwacha amekaa. Asubuhi ndipo alikutwa amefariki hapohapo. Bado hatujajua chanzo cha kifo, kwani mwili wake umehifadhiwa hospitalini kwa uchunguzi zaidi,” amesema Malongo.

Ameongeza kuwa taarifa zaidi kuhusu chanzo cha kifo pamoja na ratiba ya mazishi zitatolewa baada ya taratibu za kitabibu kukamilika.

Kifo cha Billo kimeacha pengo kubwa katika maendeleo ya soka, hususan katika kuinua vipaji vya wanawake kupitia timu yake ya Bilo Queens. Wadadau wa michezo wanatarajiwa kuendelea kutoa salamu za rambirambi huku wakikumbuka mchango wake mkubwa katika tasnia ya soka nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment