ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 16, 2026

BALAA LA YANGA KWA MBEYA CITY LEO


MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga SC yamefungwa na mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo mawili dakika ya saba na 82, kiungo Muivory Coast, Pacome Peodoh Zouzoua dakika ya 10 na 44, kiungo Mkongo Maxi Mpia Nzengeli dakika ya 16 na beki mzawa, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ dakika ya 45’+2.

Kwa ushindi huo, Yanga SC wanafikisha pointi 47 katika mchezo wa 19 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi nane zaidi ya watani, Simba SC ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi.

Kwa upande wao Mbeya City baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 17 za mechi 19 pia nafasi ya 13 kwenye ligi ya timu 16.

Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.

Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.  

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment