ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 26, 2026

MBOZI WAFANYA UCHAGUZI MWINGINE BAADA YA DIWANI ALIYEKUWEPO KUJIUWA.

 


ZOEZI la upigaji kura katika uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Shiwinga, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, linaendelea leo Februari 26, 2026, huku wananchi wakijitokeza kwa wingi.

Uchaguzi huo umeitishwa kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Lusekelo Mwalukomo, kilichotokea Novemba 26, 2025, baada ya kunywa maji ya betri, zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuapishwa rasmi kushika wadhifa huo.

Kwa mujibu wa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika kata hiyo, Selestin Luambano, jumla ya wapiga kura 6,854 wanatarajiwa kushiriki zoezi hilo katika vituo 19 vilivyotengwa kwa ajili ya kupigia kura.

Amesema jumla ya vyama nane vya siasa vimesimamisha wagombea kuwania nafasi hiyo.

Wagombea hao ni Menati Mzumbwe (CCM), Matias Dulle (ADC), Elly Shitindi (ADA-TADEA), Mary Daud (UPDP), Neema Abadallah (UMD), Emily Siwale (SAU), Mussa Dulle (Chama-Makin) na Cosam Mwakyusa (TLP).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment