Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameipa Wizara ya Maji kipindi cha wiki mbili kuhakikisha inakamilisha mchakato wa upatikanaji wa mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala.
Kwa upande wake Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema kuwa Wizara haitakuwa kikwazo katika utekelezaji wa mradi huo na watahakikisha katika kipindi cha siku 14 wanampata mkandarasi wa mradi huo.
Mradi wa maji ziwa Chala unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.66 na utanufaisha wananchi 34,104 katika vijiji 14 vya wilaya ya Rombo.
Mradi huo ambao utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 28 unapita mpakani mwa Tanzania na Kenya na unategemewa kusaidia kukuza shughuli za kijamii, kiuchumi pamoja na utalii.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Shule ya Sekondari Stephen Moshi Technical ambayo itagharimu shilingi bilioni 1.6 Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa shule hiyo ni kielelezo cha uwepo wa kiongozi mwenye maono na mipango.
Pia utahusisha uchimbaji wa kisima cha maji cha ardhini, jengo la utawala na nyumba 01 ya mtumishi.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment