
Mshambuliaji wa Mbeya City, Vitalis Mayanga amefungiwa kucheza mechi tano sambamba na kutozwa faini ya Tsh Milioni 1 kwa kosa la kumpiga kiwiko kwa makusudi beki wa kushoto wa Simba SC, Anthony Mligo.
Uamuzi huo umetolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) katika taarifa ya TPLB leo Desemba 8, 2025.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment