ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 20, 2025

JAMHURI KUJIBU PINGAMIZI LA LISSU KWENYE KESI YA UHAINI LEO.

  Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu.


Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, inaendelea kuunguruma leo Jumatatu, Oktoba 20, 2025, katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, ambapo upande wa Jamhuri unatarajiwa kuanza kujibu hoja za pingamizi zilizotolewa na Lissu.

Pingamizi hizo zinahusu upokelewaji wa video inayomuonesha Lissu akitamka maneno yanayodaiwa kuwa ya uhaini, ambayo upande wa mashtaka unataka iwe sehemu ya vielelezo vya ushahidi.

Lissu anakabiliwa na shtaka la kutoa maneno ya kuitishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinyume na kifungu cha 39(2)(d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Kesi hiyo inasikilizwa na jopo la majaji watatu likiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru, akishirikiana na majaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde.

Katika hatua hii ya usikilizwaji wa ushahidi wa Jamhuri, mahakama inatarajiwa kujibu hoja nne za pingamizi zilizowasilishwa na Lissu mnamo Oktoba 17, 2025, kuhusu kupinga vielelezo vilivyotolewa na shahidi wa tatu wa Jamhuri, akidai visipokelewe kama ushahidi halali mahakamani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment