![]() |
| Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, |
Kaganda ametoa kauli hiyo leo, Oktoba 20, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia vitendo vyovyote vitakavyolenga kuvuruga amani wakati wa uchaguzi.
“Tutawachukulia hatua za kisheria wote watakaothubutu kuhujumu zoezi la kupiga kura,” amesema Kaganda.
Aidha, amehimiza wananchi wote kushiriki kikamilifu katika uchaguzi huo akibainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kikatiba na njia muhimu ya kuchangia maendeleo ya taifa.
“Ukiamua kukaa nyumbani na usifike kupiga kura, usije kujuta baadaye. Nafasi unayo, ila ukishindwa kuitumia, utakuwa umepoteza haki yako ya msingi,” amesisitiza.
Mkuu huyo wa wilaya amewahakikishia wananchi wote wa mjini na vijijini kuwa ulinzi na usalama umeimarishwa, hivyo waende wakapige kura kwa amani na utulivu, wakitumia haki yao ya kuwachagua Rais, wabunge na madiwani wanaowataka.
Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment