ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 25, 2025

KAUSHA DAMU IMEWAFILISI WAFANYABIASHARA WENGI JIJINI MWANZA

 ALBERT G.SENGO/MWANZA

WAFANYABIASHARA mkoani Mwanza wamesema kinacho wakwamisha kuendelea kiuchumi, kukuza biashara zao ni kukithiri kwa mikopo yenye riba kubwa ‘mikopo kausha damu’. Wamesema mikopo hiyo huwafanya kushindwa kutekeleza vyema kazi zao hali inayowafanya wengi wao kufilisika na kuwa maskini. Walisema hayo juzi wakati wakizungumza na viongozi na maofisa wa benki ya Equity Bank waliofika jijini hapa kutoa mafunzo ya kuendesha biashara, kukuza mitaji kwa wanawake na wafanyabiashara. Biashara ni Maendeleo! Equity Bank Mwanza inashirikiana na wafanyabiashara kuleta suluhisho za kifedha Equity Biashara Forum, mahali pa mabadiliko. #samiasuluhuhassan #biashara #EquityBankTanzania #EquityBiasharaForum #EquiyInMwanza

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment