ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 4, 2025

DARAJA LA J P MAGUFULI (KIGONGO BUSISI) LIKO TAYARI KWA MATUMIZI

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

MSEMAJI Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Daraja la Kigogo-Busisi maarufu kama Daraja la JPM lipo tayari kwaajili ya matumizi na kuwa muda wowote kuanzia sasa watu wataruhusiwa kupita wakati likisubiri kuzinduliwa. Msigwa amebainisha hayo mnamo tarehe 3 Mei 2035 akiwa katikati ya daraja hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari alioambatana nao kwaajili ya ukaguzi wa miradi mbari mbali ya maendeleo inayotekelezwa katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga. Alisema daraja hilo linalounganisha Wilaya mbili za Sengerema na Misungwi linaunganisha pia mataifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. Alisema kuanza kutumika kwa daraja hilo kutafungua fursa za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni katika mataifa pamoja na mikoa yote inayounganishwa na daraja hilo

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.