NA ALBERT G.SENGO/MWANZA
MSEMAJI Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Daraja la Kigogo-Busisi maarufu kama Daraja la JPM lipo tayari kwaajili ya matumizi na kuwa muda wowote kuanzia sasa watu wataruhusiwa kupita wakati likisubiri kuzinduliwa. Msigwa amebainisha hayo mnamo tarehe 3 Mei 2035 akiwa katikati ya daraja hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari alioambatana nao kwaajili ya ukaguzi wa miradi mbari mbali ya maendeleo inayotekelezwa katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga. Alisema daraja hilo linalounganisha Wilaya mbili za Sengerema na Misungwi linaunganisha pia mataifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. Alisema kuanza kutumika kwa daraja hilo kutafungua fursa za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni katika mataifa pamoja na mikoa yote inayounganishwa na daraja hiloTupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.