ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 8, 2025

HADITHI YA JINSI WIMBO WA SHAGGY (IT WASN'T ME') ULIVYOTENGENEZWA.

 


The Story of 'It Wasn’t Me' by Shaggy.

Wakati Shaggy akirekodi albamu yake ya Hot Shot, yenye mikwaju kama "It Wasn't Me" na "Angel", lebo hiyo iliikataa kama albamu ya kutupa isiyo na manufaa na "hakuna hits" humo ndani yaani ni kama album ya kupoteza muda tu hivyo "It wasn't Me" haikutolewa hata kama single.

Lakini mfululizo wa ajali za kufurahisha na siyo mbaya, ikiwemo upakuaji haramu kwa njia za kiwizi na kiudukuzi mitandaoni, ilipelekea kuusukuma wimbo "It Wasn't Me" kuwa moja ya vibao vya kwanza viliyopelekwa sokoni kwa njia ya kimagendo na kugeuka kuwa muhimu kwenye menyu za ma-Dj wengi duniani.

Mtayarishaji VICE anakutana na Shaggy kwenye kumbukumbu ya miaka 20 ya album 'Hot Shot' ambayo inaambatana na kutolewa kwa albamu yake mpya kabisa ya Hot Shot 2020, na kuhadithia jinsi wimbo "It Was'nt Me" ilivyowafungulia dunia. Click here to subscribe to VICE: http://bit.ly/Subscribe-to-VICE
Kutoka katika picha za kumbukumbu mwanahabari Albert G. Sengo (left) na mwanamuziki toka nchini Marekeni 'Shaggy' alipokuja jijini Mwanza mnamo mwaka 2011 na kupiga bonge moja la show katika Tamasha la  'Serengeti Fiesta 2011'
Kabla ya kutoa burudani katika tamasha la Fiesta, Shaggy alihudhuria tamasha la asili ya watu wa kanbila la Wasukuma linaloitwa Bulabo na kusimikwa kwa kupewa hadhi ya Utemi wa Sukuma kupitia jina lake hili hilo maarufu na kuitwa "Ng'wana Shaggy"

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.