ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, October 20, 2024

MBUNGE UMMY APITA VIJIWENI KUHIMIZA WANANCHI KUJIANDIKISHA NA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

 

Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM) Mhe Ummy Mwalimu  Octoba 18 mwaka 2024 ametembelea vijiwe mbalimbali katika mitaa ya Mwambani, Mchukuuni, Mwahako, Mwakidila na Mwang'ombe katika kata za Tangasisi na Masiwani kuhamasisha wananchi kujiandikisha katika daftari la mkazi na pia kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakao fanyika tarehe 27/11/2024.


Akizungumza mara baada ya kuvitembelea vijiwe hivyo amesema  kuwa mitaa ndio chimbuko la Amani na Maendeleo kwa Wananchi hivyo ni muhimu kila wananchi wa Tanga Mjini kushiriki.
Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM) Mhe Ummy Mwalimu akisikiliza maoni ya wananchi wake, na kutathimini uelewa wao kwa masuala ya umuhimu wa uchaguzi wa serikali za mitaa.
Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM) Mhe Ummy Mwalimu akipokea mawazo ya mmoja wa vijana baada ya kutoa elimu ya umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la orodha ya uchaguzi serikali ya mtaa.
Wavuvi mpo tayari!!....Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM) Mhe Ummy Mwalimu.

Boda boda mpooo!!...
Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM) Mhe Ummy Mwalimu na wananzengo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.