ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, July 29, 2024

UVCCM YAUNGANA NA OFISI YA MKUU WA WILAYA KUCHANGIA DAMU KITUO CHA AFYA MKOANI

VICTOR MASANGU/PWANI SAUTI BY GSENGO Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu wa tano Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuokoa vifo vya mama na mtoto Ofisi ya Wilaya ya Kibaha kwa kushirikiana na Umoja wa vijana (UVCCM) Wilaya ya Kibaha mjini imemua kuendesha kampeni maalumu kwa ajili ya uchangiaji wa damu katika katika kituo cha afya Mkoani kwa lengo la kuweza kuokoa maisha ya mama na mtoto. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa amesema kwamba wameamua kwenda kuchangia damu katika kituo hicho kutokana na kuwepo kwa uhitaji mkubwa wa damu kwa wagonjwa ambao wanakwenda kupatiwa matibabu hususan kwa wakinamama wajawazito.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.