ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, June 19, 2024

RAIS SAMIA AWASILI AFRIKA YA KUSINI KUHUDHURIA UAPISHO WA RAIS RAMAPHOSA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Waterkloof Pretoria nchini Afrika Kusini tarehe 18 Juni, 2024. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais mteule wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Waterkloof Pretoria nchini Afrika Kusini tarehe 18 Juni, 2024. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais mteule wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini Dkt. Grace Naledi Pandor pamoja na Thembi Nkadimeng Waziri wa Utawala na Ushirika na Masuala ya Jadi. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais mteule wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Watanzania waishio Afrika Kusini mara baada ya kuwasili Pretoria tarehe 18 Juni, 2024. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais mteule wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.