ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 18, 2024

SIKU MBILI ZA VIPIMO VYA SARATANI NA UCHUNGUZI BURE JIJINI MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

ZAIDI ya asilimia 40 ya wanawake nchini wanakabiriwa na tatizo la Saratani ya Matiti hali inayosababisha kujitokeza vifo vingi vinavyotokana na ugonjwa huo kutokana na wagonjwa wengi kufika hospitalini hatua za mwisho. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Mradi wa Saratani ya matiti Dr. Mary Giattas katika warsha ya kuwajengea uwezo madaktari wa saratani waliopo katika Hospitali za mkoa wa Mwanza, namna ya uchunguzi wa ugonjwa huo. Tarehe 18 na 19 Juni 2024 Hospitali ya Makongoro na Buhongwa ndizo zitakazo husika na mradi huo ambapo wanawake watapata fursa ya kupata huduma ya uchunguzi wa saratani bure, ukiwa umelenga kuwafikia wanawake zaidi ya 500 katika mikoa mitatu nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.