ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 30, 2024

ZEE LA NYETI AJILAUMU KIFO CHA GADNA - "UKISIKIA MTU ANAUMWA USIAHIRISHE NENDA KAMSABAHI"

 NA ALBERT G. SENGO/ ROMBO, KILIMANJARO

Mwandishi wa Habari za Burudani na Michezo wa Gazeti la Mwananchi ambaye pia ni Mtangazaji na Mjasiliamali, Henry Mdimu 'Zee la Nyeti' amezungumza na Jembe Fm wakati wa mazishi ya mwanahabari nguli wa Clouds Fm, Gadna G. Habash, jinsi alivyoguswa na msiba wa marehemu huyo aliyefariki asubuhi ya Jumamosi ya tarehe 20 April 2024 baada ya kuugua na kulazwa katika Hospitali ya Jakaya Kikwete jijini Dar es salaam. Mdimu ameiasa jamii kutopuuzia suala la kwenda kwa wakati kuwajulia hali wapendwa wao wanapougua kwani yeye aliahirisha mara kadhaa kwenda kumtembelea hospitalini marehemu Gadna wakati alipopata taarifa za kulazwa kwake. "Nimejuta Gadna wiki moja kabla ya kifo chake nilikuwa nafanya show Morogoro kwahiyo tuklikuwa tumeshaelewana, tumeshalipana hela ya tangazo lakini kesho yake nikasikia jamaa amelazwa, nikawaambia stuff wangu msimsumbue huyu jamaa kwasababu nimetoka naye mbali, tutakuja kufanya naye tangazo siku nyingine na nikirudi Dae es salaam nitakuja kumwona" "Nimeenda Dar es salaam nimekaa siku tatu, sikupata nafasi ya kwenda hospitali lakini nilikuwa napiga simu kwa marafiki, jamani kuna mtu amekwenda kumwona Gadna?'" Jibu - "Yes" Swali - "Anaendeleaje?" Jibu - "Yuko Powa" "Basi nikasema niende tena Morogoro nikirudi nitamkuta, nafika tu Morogoro nasikia Gadna amefariki"............ #samiasuluhuhassan #mwanza #rombo #gadna

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.