ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 30, 2024

'HAYA NDIYO NILIYOYAKUTA NDANI YA HIFADHI YA MAKUMBUSHO YA AZIMIO YA ARUSHA'

 NA ALBERT G. SENGO/ ARUSHA

Napata fursa ya kutembelea Makumbusho ya Azimio la Arusha yaliyoko eneo la Kaloleni, karibu na Mnara wa Uhuru (Mnara wa Mwenge). Hadi mwaka 1967, jengo hili lilitumika kama ukumbi wa ustawi wa jamii kwa jamii ya Kaloleni jijini Arusha. Mnamo Januari 1967, jengo hilo lilikuwa na mkutano wa kihistoria ambao Sera ya Kisiasa na Kiuchumi ya Tanzania ya Ujamaa na Kujitegemea ilitolewa. Mnamo Februari 1977 jengo hilo lilibadilishwa kuwa jumba la kumbukumbu ndogo la kisiasa na uchumi. Jeh ni yapi yaliyomo ndani ya Makumbusho haya? Ungana nami msimulizi wako Albert G. Sengo nikupitishe hatua kwa hatua katika eneo hili ambalo ni nyenzo muhimu ya kufundishia kwa historia, kiraia, masomo ya jumla na masomo ya sayansi ya siasa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.