ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 22, 2023

HOTUBA YA MHE. DOTO BITEKO NAIBU WAZIRI MKUU MBELE YA MAKARDINALI NA MAASKOFU - JIMBO KUU TABORA

NA ALBERT GSENGO Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wa wananchi wa kutoa mawazo, imani na uchaguzi katika dini na hivyo itahakikisha kuwa kunakuwa amani na utulivu ili uhuru huo wa kuabudu na kutoa mawazo uwepo. Dkt.Biteko amesema hayo tarehe 19 Novemba, 2023 wakati alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Sherehe za kumpongeza Mhasham Askofu Mkuu Mstaafu Paul Ruzoka na kumpokea rasmi Askofu Mkuu Mpya wa Tabora, Mwadhama Protase Kardinali Rugambwa. Sherehe zilizofanyika katika Jimbo Kuu Kanisa Katoliki Tabora.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.