ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 10, 2023

Rais Samia Suluhu kuhudhuria Ibada ya kumbukizi ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere Mkoani Manyara.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anatarajia kuhudhuria ibada maalum ya kumbukizi ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Oktoba 14, 2023 mjini Babati - Manyara.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa katika Ibada iliyofanyika katika Kanisa la Parokia ya Roho Mtakatifu Babati imesema kuwa ibada hiyo itaanza saa 1.30 asubuhi na itaendeshwa na Mhashamu Baba Askofu Anton Lwagwen.

"Tunawaomba waumini muhudhurie kwa wingi ibada ya Kitaifa itakayofanyika kanisani kwetu, tunapata ugeni mzito ni vyema na sisi tukajitokeza kwa wingi," katibu wa kanisa.

Ibada hiyo itahudhuriwa na Mama Maria Nyerere pamoja na viongozi mbali mbali watakaokuwa wameambatana nae.

Vile vile baada ya kumaliza kwa ibada kutakuwa na hafla katika uwanja wa Tanzanite Kwara kwa ajili ya uzimaji wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.