ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 15, 2023

HII IMEENDA 'KUMBE NA RAIS SAMIA NAYE YANGA' MUSUKUMA ATETEMA KAMA MAYELE

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Wakati mashabiki na wanachama wa Yanga wakiwa na hofu juu ya hatma ya mshambuliaji wao hatari raia wa Congo DR, Fisto Mayele kama ataendelea kuwepo msimu ujao, mwanachama na Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku 'Musukuma' amedokeza alichozungumza na Rais wa Klabu hiyo, Hersi Said juu ya hatma ya mkongomani huyo. Musukuma akizungumza leo katika uzinduzi wa Wiki ya Mwananchi amesema amekuwa akifanya mazungumzo ya mara kwa mara na Rais Hersi ambaye amemuhakikishia kuwa wananchi wataendelea kupata burudani ya kutetema msimu ujao. Bila kutaja jina la Mayele, Musukuma ametumia lugha ya ishara akionyesha stairi ya ushangiliaji ya Mayele huku mashabiki na wanachama wa timu hiyo waliojitokeza katika uzinduzi huo uliofanyika Furahisha Wilayani Ilemela mkoani Mwanza wakimuunga mkono kwa kutetema.













Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.