ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 8, 2023

SHAMBA BOY AWEKA HISTORIA KUPACHIKA MIMBA MABINTI WATATU WA TAJIRI WAKE

 


Shamba boy mmoja Mkenya ambaye jina lake limehifadhiwa, ameweka historia ya kuwapachika mimba mabinti watatu wa tajiri wake.

Warembo hao watatu wana wazazi wakali ambao kwa kawaida waliwafungia ndani ya nyumba na kuwanyima nafasi ya kutangamana na marafiki.

Dada watatu wanaripotiwa kupachikwa mimba na mwanaume mmoja ambaye ni shamba boy wao

Inasemekana kuwa dada hao watatu kwa kawaida waliwekewa vikwazo na wazazi wao ambao walikuwa wagumu sana kwao na pia kuwazuia kufanya urafiki

 Wakati mama wa dada hao watatu alipogundua ukweli, alizimia papo hapo na mfanyakazi huyo alitimuliwa

Inaripotiwa kwamba mfanyakazi huyo pekee ndiye aliyekuwa akitangamana nao.

Kama ilivyoelezwa kwenye chapisho hilo, shamba boy huyo alianza kujamiana na dada wote watatu bila wazazi wao ambao ni Wakristo wenye itikadi kali kujua.

Imeelezwa  kwamba mfanyakazi huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mzaliwa wa pili na alikamatwa katika tendo hilo na dada yake mkubwa.

Wakati huo huo, ili kifungua mimba aweze kuweka siri hiyo, alimwomba shamba boy huyo kutosheleza kiu yake ya ngono.

Wakiwa wanarushana roho, mzaliwa wa tatu naye aliwafumania katika kitendo hicho na pia alidai hamu yake ya mapenzi ili kujiridhisha ikiwa hawataki awaambie wazazi wao wakali.

Matokeo ya uhusiano wao na mfanyakazi huyo yaligeuka kuwa ujauzito na wote watatu wamejifungua.

 Baada ya kusikia habari hizo, wazazi hao walipigwa na butwaa kutokana na jinsi mambo yalivyobadilika licha ya jitihada zote za kuwaepusha kutangamana na wanaume.

 Walipoulizwa ni nani aliyehusika na ujauzito huo, walimwaga mtama na kumtaja shamba boy huyo, habari ambazo zilimfanya mama yao kuanguka chini na kuzirai papo hapo.

Wazazi hao sasa wamekubali matokeo baada ya kupewa ushauri nasaha na kujilaumu kwa kuwa wakali sana kwa binti zao.

Shamba boy naye alipigwa kalamu lakini dada hao bado humtumia pesa na kumpenda kama baba wa binti zao wawili na mtoto wa kiume.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.