ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 6, 2023

BWANA HARUSI AANGAMIA BAADA YA KULIPULIWA NA BOMU LILILOTEGWA KWENYE ZAWADI


Mwanaume mmoja amefariki baada ya mfumo wa ukumbi wa michezo nyumbani aliyopokea hivi majuzi kama zawadi ya harusi kulipuka.

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, bomu hilo lilikuwa limetegwa kwenye zawadi hiyo ambalo lililipuka muda tu ilipowekwa katika umeme.

Bwana harusi huyo ambaye alikuwa pamoja na kaka yake, alifariki papo hapo huku kaka yake akifariki kutokana na majeraha alipokuwa akipokea matibabu.

Wakati huo huo watu wengine wanne, akiwemo mvulana wa miezi 18, walijeruhiwa katika mlipuko huo, ambao ulifanyika Jumatatu, Aprili 3, nyumbani kwa bwana harusi katika wilaya ya Kabirdham katika jimbo la kati la India la Chhattisgarh

Polisi wamesema mlipuko huo ulikuwa mkubwa kiasi kwamba kuta na paa la chumba hicho zilianguka kutokana na athari zake.

Bomu hilo lilidaiwa kutegwa na mpenzi wa zamani wa bibi harusi ambaye alikuwa na machungu dhidi yake kwa kuolewa na mwanamume mwingine.

Mshukiwa kwa jina Sarju Markam kutoka jimbo jirani la Madhya Pradesh alikamatwa Jumanne, Aprili 4.

Markam, 33, alikuwa na uhusiano na mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 29 na alikuwa akisisitiza kuwa awe mke wake wa pili.

Lakini familia ya mwanamke huyo ilikataa na kupanga ndoa yake mahali pengine.

Bwana harusi amtema bibi harusi madhabauni

Baada ya kugundua swala la kuhuzunisha kuhusu mke wake siku ya harusi yake, bwana harusi amefutilia mbali mipango ya ndoa.

Mwanaume  huyo aligundua kwamba mrembo wake tayari alikuwa na watoto wawili na mwanamume mwingine.

Bwana harusi huyo ameelezea uchungu wake alipofuta mipango ya harusi na kuvua viatu vyake vya harusi na suti.

Licha ya juhudi kadhaa ya walioshuhudia kumtuliza, bwana harusi aliyekuwa amepandwa na mori alikataa kuendelea na harusi.

Pia alidai kurejeshewa mahari aliyolipa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.