ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 6, 2023

ANUSURIKA KUFA BAADA YA KUJIKATA NYETI


Mwanaume aitwaye Anselumu Sebuka, miaka 42, Mkulima na mkazi wa Namagondo  wa kitongoji cha Kasuzu, kijiji na kata ya Namagondo, tarafa ya Mumulambo wilayani Ukerewe  alikutwa ndani ya chumba chake akiwa amejaribu kujiua kwa kukata uume wake kwa kutumia kisu chenye ncha kali.

Inadaiwa Ansele Sebuka alikuwa anatuhumiwa na ndugu zake kuiba mali mbalimbali za familia yake na za jamii inayomzunguka na kwenda kuziuza pamoja na ulevi uliokithili ambapo waliamua kumtenga kutokana na tabia zake.

Baada ya tuhuma hizo ndipo aliamua kujikata uume wake kwa kisu na kuacha unaning’inia kwa lengo la kujiua.

 Chanzo cha tukio hilo ni ugonvi wa kifamilia uliopelekea mhanga kupata msongo wa mawazo.

Ansele Sebuka alipelekwa katika Hospitali ya wilaya ya Ukerewe kwa ajili ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kufuata njia sahihi za kutatua matatizo yao hususani kuwaona wataalamu wa afya ya akili ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na msongo wa mawazo na kukosa uvumilivu wa migogoro mbalimbali katika jamii.

 Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi badala yake watumie njia sahihi katika kuhakikisha wanatatua matatizo yao bila kuleta madhara na usumbufu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.