ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 10, 2023

TASAC YATOA MAFUZO KWA WADAU WA SERIKALI JUU YA MABADILIKO YA KANUNI KATIKA KUDHIBITI VIVUKO VYA SERIKALI

 

Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limeanza kutoa Mafunzo kwa wasimamizi wa Sheria Mkoani Mara ikiwa ni Mkakati wa kujua Mabadiliko ya Sheria mbalimbali za Shirika hilo ambalo kwasasa limepewa jukumu la kusimamia vivuko hapa nchini.

Mkuu wa wilaya ya Musoma Dkt Khalfan Haule amefungua mafunzo hayo na kusema juu ya umuhimu wa kujua Mabadiliko hayo ni ili kutekeleza Majukumu ya usimamizi wa Sheria kwa Haki katika usalama wa Wananchi na Vyombo vya usafiri Majini.





Aidha, Afisa Mfawidhi TASAC Mkoa wa Mara na Simiyu Abed Mwanga amesema zamani vivuko hivyo vilikuwa chini ya sheria ya SUMATRA lakini kwasasa vitasimamiwa na TASAC kwa mujibu wa Sheria na TASAC itaendelea kutoa mafunzo hayo kwa wadau mbalimbali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.