ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, February 6, 2023

NI VILIO TU.

 Vilio simanzi na uzuni zimetanda kwa wananchi wa wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro wakati wa shughuli za kuaga miili ya watu 12 waliofariki kwa ajali ya gari Februari 3 mwaka huu katika eneo la Magira Gereza wilayani Korogwe mkoani Tanga wakati wakielekea Rombo kwa mazishi ya Atanas Mrema.


 "Msiba huu ni mkubwa ambao hauwezi kuelezeka hivyo niwape pole wananchi wa Rombo hasa wanafamilia kutokana na kuondokewa na ndugu zenu niwaombe mjipe moyo katika kipindi hiki kigumu" Nurdin Babu RC Kilimanjaro.


 "Tunayo majonzi makubwa wanakilimanjaro na tunachopaswa ni kumuomba Mwenyezi Mungu atutie nguvu katika kipindi hiki cha majonzi na tuwaombee ndugu zetu wapumzike mahali pemapeponi" Nurdin Babu RC Kilimanjaro.
 "Niwaombe viongozi wa dini kufanya maombi makubwa katika nyumba za Ibada ili kuepusha ajali zinazopeleka vifo vya watu" Nurdin Babu RC Kilimanjaro.

 "Jeshi la Polisi endeleeni kutoa elimu kwa madereva kufuata sheria za barabarani kwani wapo baadhi ya madereva wamekuwa hawafuati alama na sheria za barabarani hali inayopelekea vifo vya watu kutokana na ajali" Nurdin Babu RC Kilimanjaro.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.